Usalama Na Afya
Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe
The easy, fast & fun way to learn how to sing: 30DaySinger.com
As long as unapewa chako unatembea/ Iwe mshahara au kifuta jasho unapokea/ Na kesho unarudi tena na kazi inaendelea/ Ndo unajikuta unafanya kazi kimazoea/ Cha msingi mkono uende kinywani/ (au sio) na watoto waende uani/ (namna hiyo) , muhimu unaingiza cash flani/na kazi ni halali wala haijalishi kazi gani/ Ndivyo ilivyo vivo hivyo hilo liko wazi man/ Ila jiulize kazi yako ina usalama kiasi gani/ Yaani! Mazingira ya kazi yakoje/ Ni salama au kuna hatari yoyote/ Sio sababu haujawahi kudhurika/ Ndio iwe guarantee kuwa hupaswi kujiuliza/ Majuto ni mjukuu ni vizuri ukabadili/ Usiishie kuridhishwa na kauli ya mwajiri/ Yeah! Kauli ya tajiri au bosi/ Bila wewe kuchunguza mazingira haitoshi/ Hili swala ni la kufanyia kazi kwa pamoja/ Ni lazima kuzuia ajali na magonjwa/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini Kwa kuwa bado mapema yani bado alfajiri/ Well.. Ngoja nianze na mwajiri/ Kama sheria peke yake inatosha unatuambia/ Mbona kuna watu wanakufa na kuumia/ Law pekee hazileti usalama kazini/ Ni wajibu kujilinda na kuwalinda wengine/ Toa mafunzo kwa miaka miwili mara moja/ Kila mtumishi ahudhurie bila kukosa/ (ili) aelimishwe anayofaa kutekeleza/ Iwe vifaa au mashine anayofaa kuendesha/ Wape tahadhari toa maelezo na maagizo/ Waingie salama na kutoka hivyo hivyo/ Weka vifaa vya usalama kwa kila mtu/ Maana afya na usalama ni haki ya kila mtu/ukiwa mwajiri ni lazima/ Utoe kifaa cha kinachofaa cha kulinda, ikiwa wafanyakazi wanaachwa wazi kwa mazingira ya kuumiza.. Ppe wanaita/ yeah! Na ppe inayohitajika inatofautiana kulingana na kazi inayofanyika/ Kusiwe na hatari ya kitu chochote/ Iwe vifaa, wanyama, ama sumu yoyote/ Na pia.. Hakikisha usafi unaostahili/ Toa maji kwa wingi/ Na idadi ya kutosha ya vyoo nayo ya msingi/ Na pia mahali wanapobadili nguo wafanyakazi , na mahali wanakopumzika wafanyakazi nako ni muhimu pawe safi na sahihi/ Na kumbuka, unapowafanyia yote hayo/ Sio ruhusa kuwakata kwenye mishahara yao/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini/ Hakikisha usalama na afya kazini/ Usalama na afya kazini Baada ya vingi vya kumwambia/ Bosi.. Nafunga kipindi na waajiriwa/ Kwanza.. Msipende mambo ya kurahisisha/ Msianze kwanza kazi kabla ya kuhakikisha/ Uzima wa miundo mbinu hadi milango madirisha/ Vyumba vina hewa na mwanga wa kuridhisha/ Kisha vaeni vifaa vya kujilinda/ Hata kama vinachosha ila vitawakinga/ Na msione ka karaha ndogo ndogo/ Mkishatumia msiache vifaa hovyo hovyo/ kama kuna maji yanamwagika yakaushwe/ Kama kuna vumbi linazalishwa lifutwe/ Kumbuka na kuzima unapowasha umeme/ Na kama kuna nyaya zimechubuka useme/ Usisite kuripoti unapoona tatizo/ Usipuuze chochote upewapo angalizo/ (na ni hatari) kufanya kazi kupindukia/ Nchi nyingine hichi ni kinyume na sheria/ Mtu aliyechoka ni rahisi kukosea/ Haya sio maneno yangu ni tafiti zinaongea/ Usiume kisa unataka ufanyakazi bora/ Ofisi haikui kwa vifo na wafanyakazi wagonjwa/ Hadi hapo sina kingine cha kusema/ Nimemaliza zaidi niwatakie kazi njema/
Become A Better Singer In Only 30 Days, With Easy Video Lessons!
Citation
Use the citation below to add these lyrics to your bibliography:
Style:MLAChicagoAPA
"Usalama Na Afya Lyrics." Lyrics.com. STANDS4 LLC, 2024. Web. 20 May 2024. <https://www.lyrics.com/lyric-lf/11654408/Micshariki+Africa+%26+Adam+Shule+Kongwe/Usalama+Na+Afya>.
Discuss the Usalama Na Afya Lyrics with the community:
Report Comment
We're doing our best to make sure our content is useful, accurate and safe.
If by any chance you spot an inappropriate comment while navigating through our website please use this form to let us know, and we'll take care of it shortly.
Attachment
You need to be logged in to favorite.
Log In